Majaliwa awasili Belarus

0

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa Julai 21, 2025 amewasili nchini Belarus kuanza ziara ya kikazi nchini humo.

Kwenye Uwanja wa Ndege wa Kinsk alipokelewa na Naibu Waziri Mkuu wa Beralus, Viktor Karankevich.

Katika ziara hiyo siku ya kwanza, Waziri Mkuu ataweka shada la maua katika mnara wa mashujaa wa Jamhuri ya Beralus.

Pia, atatembelea kiwanda cha kutengeneza Matrekta na vifaa mbalimbali vya kilimo (Minsk Tractor Plant) na baadae atakutana na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Belarus Alexander Turchin.

Katika ziara hiyo ameambatana na Balozi wa Tanzania Urusi na Belarusi, Frederick Ibrahim Kibuta, Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Shariff Ali Shariff na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Cosato Chumi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here