Ousmane Dembele
VYANZO mbalimbali vya habari vya Kimataifa vinaripoti kuwa, Kombe la Dunia limebadili mwelekeo wa mbio za tuzo za Ballon d’Or, huku Lamine Yamal akitajwa kuwa ni miongoni mwa watakaogombea tuzo hizo kwa mwaka huu.
Yamal ni mmoja wapo wanaopendekezwa zaidi kushinda taji la Ballon d’Or 2026, ambapo ushindi wa Kombe la Dunia unampa nafasi kubwa ya kushinda Ballon d’Or, ingawa bado ana mapungufu katika rekodi yake ya mwaka huu.
Winga huyo wa Barcelona alitolewa kwenye hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, jambo linalomaanisha hawezi kujivunia kushinda mataji mawili makubwa zaidi katika ngazi ya klabu na timu ya Taifa ndani ya mwaka mmoja.
Ousmane Dembele, anayetetea tuzo yake anaingia katika hatua ya mwisho ya mchujo akiwa na medali ya ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, lakini alitolewa kwenye nusu Fainali ya Kombe la Dunia, jambo lililodhoofisha jitihada zake za kutetea tuzo hiyo.
Kylian Mbappe na Lionel Messi bado wako kwenye mbio za tuzo hiyo, huku Messi akiiongoza Argentina hadi fainali kabla ya kushindwa katika hatua ya mwisho. Mbappe alitwaa Kiatu cha Dhahabu baada ya Messi kushindwa kuiongoza Argentina katika fainali.
Ballon d’Or ni tuzo ya kifahari zaidi ya mchezaji binafsi wa soka duniani. Tuzo hiyo ilianzishwa mwaka 1956, na hakuna zawadi ya moja kwa moja ya fedha inayotolewa, lakini inampa mchezaji umaarufu mkubwa unaomwezesha kupata mikataba minono ya kibiashara na timu au wadhamini.