WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa amesema hadi Machi, 2025 Shilingi Trilioni 1.11 zimekusanywa sawa na asilimia 93.15 ya lengo la kukusanya Shilingi Trilioni 1.60 kwa Mwaka 2024/25.
Akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi hiyo kwa Mwaka 2025/26, Waziri Mchengerwa amesema kati ya fedha hizo Shilingi Tilioni 61.21 ni kodi ya majengo, Shilingi Trilioni 1.04 ni mapato ya ndani ya mamlaka za Serikali za mitaa.
Pia, alisema Shilingi Bilioni 16.23 ni mapato ya ndani ya taasisi na Shilingi Milioni 201.60 ni maduhuli ya mikoa.
Amefafanua kuwa makusanyo hayo yalitokana na ada za wanachuo, tozo, ukusanyaji wa madeni, mauzo ya bidhaa mbalimbali na ushuru unaotozwa na mamlaka za serikali za mitaa kulingana na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa, Sura 290.
Mchengerwa alisema, kwa kipindi hicho TAMISEMI ilipanga kutumia Shilingi Bilioni 541.27 za mapato ya ndani ya halmashauri kwa ajili ya kuchangia utekelezaji wa shughuli za maendeleo. Hadi Machi, 2025 Shilingi Bilioni 312.30 sawa na asilimia 57.70 zimetolewa.
Ameeleza kuwa baadhi ya miradi iliyotekelezwa kwa kipindi hicho ni ujenzi wa miundombinu ya elimu, afya, ujenzi wa barabara, machinjio, minada nyumba za walimu na watumishi wa afya, hospitali, vituo vya afya, zahanati, vituo vya polisi, ununuzi wa magreda