RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema ni muhimu kuzinduliwe mpango wa ujuzi wa Vijana wa Jumuiya ya Madola ambao utawapa vijana milioni moja ujuzi katika sekta ya uchumi wa bluu na kijani ifikapo 2030.
Rais Dkt. Mwinyi alisema hayo alipozungumza katika Mkutano wa Biashara na Uwekezaji wa Jumuiya ya Madola (Commonwealth Trade & Investment Summit 2025) kwenye ukumbi wa Jiji la kihistoria Mansion House, London unapofanyika mkutano huo Aprili 7, 2025.
Amehimiza kuanzishwa kwa ufadhili wa kujitolea na utaalam katika sekta hiyo ili kuharakisha maendeleo endelevu ya bahari katika nchi za Jumuiya ya Madola.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi ametoa wito kwa washiriki wa mkutano huo kuitembelea Zanzibar na kujionea fursa za uwekezaji katika sekta ya uchumi wa buluu, utalii wa mazingira, nishati mbadala ya bahari, ufugaji wa samaki endelevu na maendeleo ya bandari.
Kwa upande mwingine, Rais Dkt.Mwinyi alisema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo Mwaka 2050 Zanzibar itakuwa ya uchumi wa kati baada ya kuzinduliwa kwa Dira ya Maendeleo kupitia mkakati wa sera ya uchumi wa buluu ya Mwaka 2022.
Mkutano huo umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali kutoka Nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola.