Rais Samia aongoza hafla ya kutoa heshima ya mwisho kwa Rais Mstaafu Mwinyi

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akiwa pamoja na Viongozi mbalimbali katika uwanja wa Michezo wa Amani mjini Zanzibar kwa ajili ya kuongoza Viongozi na Wananchi wa Zanzibar kutoa Heshima za mwisho kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi aliyefariki dunia Februari 29, 2024 katika Hospitali ya Mzena Jijini Dar es salaam alipokuwa amelazwa akipata matibabu ya Saratani ya Mapafu, ambapo anatarajiwa kuzikwa Kijijini kwake Mangapwani Mkoa wa Kaskazini Unguja Machi 2,2024.
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ waliobeba Jeneza lenye Mwili wa Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi wakiwasili katika Uwanja wa Michezo wa Amani mjini Zanzibar Machi 2,2024.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi wakati wa Hafla ya kutoa Heshima za mwisho kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi katika uwanja wa Michezo wa Amani mjini Zanzibar.
Wajane wa Hayati Rais Mstaafu awamu ya pili Mzee Ali Hassan Mwinyi Bibi Siti Mwinyi na Khadija Mwinyi wakiwasili katika Uwanja wa Michezo wa Amani mjini Zanzibar.
Viongozi Wastaafu mbalimbali wakiwa katika uwanja wa Michezo wa Amani mjini Zanzibar kwa ajili ya kutoa Heshima za mwisho kwa Rais Mstaafu wa awamu ya pili Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here